Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF imetoa mwito wa dharura wa kuisaidia Ethiopia kukabili tatizo la utapiamlo

UNICEF imetoa mwito wa dharura wa kuisaidia Ethiopia kukabili tatizo la utapiamlo

Hilde Johnson, Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) aliwaambia wafadhili wa kimataifa mjini Geneva mnamo 26 Juni (2008) kwamba hali ya watoto katika Ethiopia ni ya kushtusha sana na ya hatari, kutokana na ukame uliotanda nchini humo kwa muda mrefu ikichanganyika pamoja na matatizo ya kupanda kwa bei za chakula.