Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mradi wa PACE umepitishwa na Mkutano wa Bali

Mradi wa PACE umepitishwa na Mkutano wa Bali

Wajumbe wa kimataifa waliokutana wiki hii kwenye mji wa Bali, Indonesia kuzingatia Mkataba wa Basel juu ya udhibiti bora wa taka za vifaa na zana za elektroniki wameafikiana kuanzisha mradi mpya utakaojulikana kama mpango wa PACE. Mradi wa PACE unatarajiwa kuandaa mwongozo maalumu wa kiufundi juu ya namna ya kurejeleza matumizi ya zile kompyuta zilizokwishatumika, hasa katika matengenezo madogo madogo na kwenye huduma za vipimo vya kisasa vya kompyuta, ili kutathminia matumizi ya vifaa hivyo vya elektroniki havitochafua mazingira.~