Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNESCO kuanzisha muungano wa manispaa za kimataifa dhidi ya ubaguzi

UNESCO kuanzisha muungano wa manispaa za kimataifa dhidi ya ubaguzi

Kwenye Warsha juu ya Haki za Binadamu unaofanyika Nantes, Ufaransa kulianzishwa na Shirika la UM juu ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jumuiya mpya ya muungano wa miji ya kimataifa, itakayoshirikisha manispaa za miji hiyo kwenye juhudi za kuandaa mitandao itakayoshughulikia juhudi za kuimarisha sera bora za kupiga vita kipamoja ubaguzi wa rangi na, kutunza tabia ya kuheshimiana, kwa kupendekeza kusuluhisha matatizo ya ubaguzi wa rangi kwa mazungmumzo badala ya adhabu, na kuhakikisha pia tamaduni tofauti au tabia anuwai zilizoselelea kwenye maeneo yao zinaruhusiwa kustawi bila ya pingamizi. ~