Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mataifa masikini yapatiwa vipimo vya kisasa kutambua haraka TB sugu

Mataifa masikini yapatiwa vipimo vya kisasa kutambua haraka TB sugu

Mashirika ya Kimataifa – ikijumuisha Shirika la Afya Duniani (WHO), Ushirikiano wa Kukomesha TB, UNITAID na Taasisi ya Kisasa ya Kubainisha Magonjwa Mapya – yametangaza kipimo kipya cha afya kutumiwa na mataifa masikini kutambua haraka zaidi ugonjwa wa kifua kikuu usiokubali tiba ya madawa ya mchanganyiko (yaani maradhi ya TB-MDR). Vipimo hivi vitatumiwa katika mataifa yanayoendelea 16, na vina uwezo wa kubainisha maradhi baada ya siku mbili tu, badala ya miezi mitatu, kama ilivyokuwa ikifanyika katika siku za nyuma.