Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM amenasihi Mataifa kuharakisha Mkataba mpya kudhibiti bora uchafuzi wa hali ya hewa

KM amenasihi Mataifa kuharakisha Mkataba mpya kudhibiti bora uchafuzi wa hali ya hewa

Ijumapili KM Ban Ki-moon alihutubia Chuo Kikuu cha Kyoto, Ujapani kwenye mhadhara maalumu uliokusanyisha mamia ya wanafunzi, wasomi na wawakilishi wa sekta binafsi, pamoja na jumuiya za kiraia. Kwenye risala yake KM alikumbusha juu ya umuhimu wa kuyahamasisha Mataifa Wanachama kushirikiana, kidharura, kwenye zile kadhia zitakazosaidia kufikia mapatano mapya mnamo mwisho wa 2009, kama ilivyokubaliwa naMkutano wa Bali mwaka jana.