Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MINURSO imeongezewa muda na BU kutuliza hali Sahara Magharibi

MINURSO imeongezewa muda na BU kutuliza hali Sahara Magharibi

Baraza la Usalama pia limepitisha, kwa pamoja, azimio la kuongeza muda wa kazi za Shirika la MINURSO katika eneo la Sahara ya Magharibi hadi Aprili 30 mwakani. MINURSO ni shirika la ulinzi wa amani la UM, liliodhaminiwa madaraka ya kufuatilia kusitishwa kwa hali ya mapigano baina ya Morocco na Chama cha Wazalendo wa Sahara Magharibi cha Frente Polisario. Vile vile MINURSO inatarajiwa kutayarisha mazingira yanayoridhisha ili kuweze kufanyika kura ya maoni kwenye eneo hilo la Afrika Kaskazini.