Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO inahimiza mataifa yazingatie haraka udhibiti wa maradhi yanayoua watoto kwa wingi

WHO inahimiza mataifa yazingatie haraka udhibiti wa maradhi yanayoua watoto kwa wingi

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetoa ripoti yenye kuihimiza jamii ya kimataifa kuendelea kuhudumia shughuli zinazohusika na udhibiti bora wa magonjwa ya kuambukiza yanayoumiza zaidi watoto wachanga, hususan ile homa ya vichomi na maradhi ya kuharisha. Mwito huu ulitolewa baada ya kugundulikana katika kipindi cha karibuni mchango mkubwa wa huduma za afya umeonekena ukitumiwa kwenye shughuli za kudhibiti UKIMWI, kifua kikuu na malaria na yale maradhi ya kuambukiza yenye kuathiri zaidi watoto yameonekana kutengwa na kutopewa umuhimu unaostahiki.