Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkataba wa Haki za Walemavu waridhiwa rasmi kimataifa

Mkataba wa Haki za Walemavu waridhiwa rasmi kimataifa

Ijumamosi ya tarehe 03 Mei 2008 Mkataba wa UM juu ya Haki za Watu Walemavu ulithibitishwa na kuidhinishwa kuwa chombo rasmi cha sheria ya kimataifa, mwezi mmoja tu baada ya taiifa la ishirini kuuridhia mkataba, ambao unatarajiwa kuwahakikishia watu walemavu milioni 650 duniani kuwa haki zao zinatambuliwa na kuheshimiwa. Mkataba wa Haki za Walemavu umeshatiwa sahihi na nchi wanchama 127 na kuridhiwa na mataifa 25 – Jamaika ikiwa nchi ya awali kufanya hivyo, wakati sahihi ya taifa la Ecuador ndio iliyouruhusu Mkataba kufanywa chombo rasmi cha Sheria ya Kimataifa.