Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM ashtumu vikali vurugu liliozuka Khartoum mwisho wa wiki

KM ashtumu vikali vurugu liliozuka Khartoum mwisho wa wiki

KM Ban Ki-moon "ameshtumu vikali vitendo vya kutumia mabavu vilivyoendelezwa na jeshi la mgambo la kundi la JEM kwenye vitongoji vya mji mkuu wa Khartoum, Sudan" mnamo mwisho wa wiki. Kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na msemaji wa KM Ban, ilisisitizwa ya kwamba utumiaji mabavu na makundi yenye silaha kusuluhisha tatizo la kisiasa ni kitendo kisiokubalika na jamii ya kimataifa kuitatua migogoro iliokabili Sudan sasa hivi, hasa ilivyokuwa vitendo hivyo vinahatarisha zaidi usalama na amani ya raia.