Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkataba wa Kulinda Haki za Walemavu unasherehekewa na Baraza Kuu

Mkataba wa Kulinda Haki za Walemavu unasherehekewa na Baraza Kuu

Baraza Kuu la UM lilikusanyika kwenye Makao Makuu kwenye sherehe maalumu ya kuwaheshimu na kuwatambua wale wajumbe wajasiri wa kutoka Serikali Wanachama kadha, wakichanganyika na jamii ya watu walemavu pamoja na watumishi wa Taasisi kadha wa kadha za UM, kwa juhudi zao za muda mrefu ambazo zilifanikiwa kuwasilisha Mkataba mpya wa Kimataifa juu ya Haki za Watu Wenye Ulemavu pamoja na Itifaki ya Khiyari. Karibuni Mkataba wa Walemavu Duniani uliidhinishwa rasmi kuwa chombo cha sheria ya kimataifa, na utatumiwa kudhamini na kulinda haki za walemavu milioni 650 wanaoishi katika sehemu mbalimbali za ulimwengu.