Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mavuno ya mpunga yanabashiriwa muongezeko mkubwa katika 2008

Mavuno ya mpunga yanabashiriwa muongezeko mkubwa katika 2008

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limeripoti kwamba mavuno ya mpunga katika mataifa ya Asia, Afrika na Amerika ya Latina yataongezeka kwa asilimia 2.3 katika 2008, muongezeko ambao utakiuka tani milioni 600 ziada. Hata hivyo bei ya mchele katika soko la kimataifa inakhofiwa itaendelea kuwa ya kiwango cha juu kabisa, kwa sababu nafaka hizo hazitomalizika kuvunwa mpaka mwisho wa mwaka.