Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tume ya kudhibiti mifumko ya bei ya chakula ulimwenguni inakutana Makao Makuu

Tume ya kudhibiti mifumko ya bei ya chakula ulimwenguni inakutana Makao Makuu

Ijumatatu asubuhi KM Ban Ki-moon aliongoza, kwa mara ya kwanza, mashauriano muhimu na wawakilishi wa tume maalumu iliodhaminiwa madaraka ya kuandaa ajenda ya mkutano mkuu utakaofanyika mwezi ujao mjini Roma, Utaliana kuzingatia hatua za kuchukuliwa na Nchi Wanachama, kudhibiti bora tatizo la mifumko ya bei za nafaka kwenye soko la kimataifa. Tume inajumuisha mashirika yote ya UM yanayohusika na shughuli za maendeleo na misaada ya kiutu, na pia Benki Kuu ya Dunia, Shirika la Fedha la Kimataifa na Shirika la Biashara Duniani (WTO).