Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Myanmar yanasihiwa kurahisisha huduma za msingi kwa waathiriwa wa kimbunga

Myanmar yanasihiwa kurahisisha huduma za msingi kwa waathiriwa wa kimbunga

Ijumatatu mjini Bangkok, Thailand, kwenye mkutano wa mashirika ya UM na waandishi habari juu ya misaada ya dharura kwa Myanmar, kulitolewa onyo na UM lenye kuitahadharisha Serikali ya Myanmar ya kuwa idadi kubwa ya raia huenda ikaangamia kwenye maeneo yalioharibiwa na Kimbunga Nargis pindi wenye madaraka hawatorahisisha uwezo wa wataalamu wa kimataifa wanaohudumia misaada ya dharura, kuwafikia, haraka, waathiriwa wa maafa ya tofani, ambao wametawanyika katika sehemu mbalimbali za nchi.