Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ITU imeripoti kukithiri kwa wateja wa simu za mkononi Afrika

ITU imeripoti kukithiri kwa wateja wa simu za mkononi Afrika

Hamadoun Toure, Katibu Mtendaji wa Shirika la UM juu ya Mawasiliano ya Kisasa (ITU) ambaye hivi sasa yupo Cairo, Misri akihudhuria maonyesho ya maendeleo ya viwanda vya mawasiliano, alinakiliwa akisema kwamba mnamo miaka mitatu iliopita bara la Afrika liliongoza katika matumizi ya huduma za mawasiliano ya simu. Kwa mujibu wa ripoti za ITU huduma za sekta ya simu katika Afrika ziliongezeka kwa kiwango kisichotarajiwa, mathalan, mwaka jana watu milioni 65 walisajiliwa kuwa wateja wapya wa simu za mkononi.