Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM umeahidi kuisaidia Uchina kukabiliana na athari za zilzala

UM umeahidi kuisaidia Uchina kukabiliana na athari za zilzala

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti kwamba imeitumia Serikali ya Uchina barua maalumu ilioahidi kwamba UM umejiandaa kupeleka wataalamu wanaohusika na huduma za haraka za maafa ili kuchangia juhudi za kuwasaidia, kihali na mali, waathiriwa wa zilzala iliopiga eneo la kusini-magharibi ya Uchina Ijumanne. Zilzala hiyo, tumearifiwa, imeshauwa maelfu ya watu, idadi ambayo inakhofiwa huenda ikaongezeka kwa kima kikubwa kabisa baadaye.