Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM akutana na wawakilishi wa ASEAN kuzingatia Myanmar

KM akutana na wawakilishi wa ASEAN kuzingatia Myanmar

KM Ban Ki-moon alimaliza mashauriano muhimu Ijumatano usiku na wawakilishi wa kutoka Mataifa Wanachama wa Umoja wa ASEAN, walio jirani na Myanmar, na vile vile kujumuisha wawakilishi wa yale mataifa wafadhili kuzingatia hali katika Myanmar na kuzingatia hatua za kuchukuliwa, kidharura, kuharakisha misaada maridhawa inayotakikana kunusuru maisha ya umma ulioathirika na Kimbunga Nargis katika Myanmar. Wajumbe hawa waliafikiana kuitisha kikao maalumu mwezi ujao cha kuchangisha msaada unaotakikana kuihudumia Myanmar kufufua tena shughuli zake za kiuchumi na kijamii kwa maendeleo ya umma, kwa ujumla.