Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM inawapatia lishe bora watoto 44,000 wa Usomali

UM inawapatia lishe bora watoto 44,000 wa Usomali

UM unaendelea kuhudumia kidharura chakula watoto 44,000 waliopo kwenye kambi za wahamiaji wa ndani ya nchi katika Usomali. Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) ndilo linaloongoza katika huduma hizi za kuwapatia watoto lishe ya kunusuru maisha, licha ya kuwa wafanyakazi wake hukabiliwa na vizingiti aina kwa aina katika operesheni zao, ikijumuisha upungufu wa usalama na mioundombinu halisi ya kurahisisha kadhia ya kugawa misaada ya kihali kwa mafanikio kwa umma muhitaji.