Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IFRC inayaombea Uchina, Myanmar na Ethiopia misaada ya dharura

IFRC inayaombea Uchina, Myanmar na Ethiopia misaada ya dharura

Shirika la Msalaba Mwekundu na Hilali Nyekundu (IFRC) Ijumaa, mjini Geneva, limeanzisha kampeni maalumu ya kuchangisha msaada wa fedha zinazohitajiwa kuendeleza shughuli zake kidharura katika Myanmar, Uchina na pia Ethiopia. IFRC iliripoti itahitajia msaada wa dola milioni 20 kuhudumia kihali aila 100,000 walionusurika na zilzala katika Uchina; dola milioni 50 kuusaidia umma uliosibiwa na madhara ya Kimbunga Nargis katika Myanmar; na vile vile dola milioni 1.7 kuhudumia chakula Ethiopia. ~