Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UNHCR azuru kambi za wahamiaji wa Usomali Yemen

Mkuu wa UNHCR azuru kambi za wahamiaji wa Usomali Yemen

Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) ambaye hivi sasa anafanya ziara rasmi nchini Yemen, aliripotiwa akitoa mwito maalumu kwa wahisani wa kimataifa kufadhilia msaada wa fedha maridhawa,za dharura, kuwahudumia kihali wahamiaji wa Usomali wanaoishi kwenye kambi za muda nchini Yemen, umma ambao ulihajiri makwao kujiepusha na mapigano yalioselelea nchini katika miaka ya karibuni. Mwito huu ulitolewa baada ya Guterres kuzuru Kambi ya Karaza ambapo wahamiaji 10,500 wa Usomali huishi, eneo liliopo kilomita 140 magharibi ya mji wa Aden.