Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ASEAN kuanzisha tume ya kuharakisha misaada ya kiutu Myanmar

ASEAN kuanzisha tume ya kuharakisha misaada ya kiutu Myanmar

Wajumbe wa Umoja wa Mataifa ya Kusini-Mashariki ya Asia, yaani Umoja wa ASEAN waliokutana Singapore, leo wameafikiana kuanzisha tume maalumu itakayodhaminiwa madaraka ya kurahisisha ugawaji wa misaada ya dharura, ya kihali, kutoka wafadhili wa kimataifa kwa Myanmar, tume ambayo itaongozwa na KM wa Umoja wa ASEAN, kwa madhumuni ya kuondosha wasiwasi wa wenye mamlaka kuhusu dhamira hasa ya michango ya baadhi ya mataifa ambayo huyatafsiri adui. Tume hiyo inatarajiwa kushirikiana, kwa karibu zaidi, na UM katika kuongoza huduma za kiutu nchini Myanmar.