Huduma za kiutu za UM zaendelea kuokoa waathiriwa wa kimbunga Myanmar
John Holmes, Naibu KM juu ya Misaada ya Dharura na Masuala ya Kiutu leo alioanana na wenye mamlaka nchini Myanmar ambapo aliwaomba wakuu wa Serikali kukuza haraka ushirikiano wao na UM, pamoja na mashirika ya kimataifa, ili waweze kuhudumia misaada ya kiutu kwa watu milioni 2.4 waliodhurika na Kimbunga Nargis.