Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahamiaji waliopo Yemen wanaombewa misaada ziada na UNHCR

Wahamiaji waliopo Yemen wanaombewa misaada ziada na UNHCR

Kwenye mkutano wa siku mbili uliofanyika kwenye mji wa Sana\'a, Yemen kuzingatia juhudi za kimataifa za kuwapatia hifadhi bora wahamiaji wanaovushwa kimagendo kwenye Ghuba ya Aden kutoka Pembe ya Afrika, kikao ambacho kilikamilisha mijadala yake hii leo, kulitolewa ombi la dharura na Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) Antonio Guterres aliyoitaka jumuiya ya kimataifa kuharakisha, na pia kuongeza mchango wao, unaohitajika kuwasaidia wahamiaji hawa kunusuru maisha.