Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM azuru maeneo yaliogharikishwa na tufani Myanmar

KM azuru maeneo yaliogharikishwa na tufani Myanmar

KM Ban Ki-moon amewasili Myanmar Alkhamisi ambapo alikutana, kwa mashauriano na Waziri Mkuu, Jenerali Thein Sein na pia mawaziri wengineo ambao walisailia taratibu za kuchukuliwa kipamoja katika kuharakisha ugawaji wa misaada ya kihali kwa umma waliodhurika na janga la Kimbunga Nargis liliolivaa taifa hilo wiki tatu nyuma. Alasiri KM alipata fursa ya kuzuru eneo la Delta la Irrawaddy, na kujionea mwenyewe binafsi athari za uharibifu wa Kimbunga Nargis kieneo.