Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la HRC lazingatia mzozo wa chakula duniani

Baraza la HRC lazingatia mzozo wa chakula duniani

Baraza la Haki za Binadamu (HRC) Alkhamisi mjini Geneva lilifanyisha kikao maalumu, kusailia mzozo wa mifumko ya bei za chakula duniani. Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu, Louise Arbour kwenye hotuba yake ya ufunguzi altahadharisha kwamba bila ya, kwanza, kulitatua tatizo la chakula kwa suluhu ya jumla, na ya kuridhisha, itakayozingatia kihakika haki za ule umma maskini, uliotengwa na kudharauliwa kwenye jamii zao, kuna hatari zile juhudi zote za kuudhibiti mzozo huu kimataifa kwenda arijojo mathalan miporomoko ya vipande vya dhumna.