Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa Mapitio ya Mapatano ya Durban kufanyika mwakani Geneva

Mkutano wa Mapitio ya Mapatano ya Durban kufanyika mwakani Geneva

Baada ya mvutano wa majadiliano miongoni mwa wanadiplomasiya wa kimataifa, wanachama wa Kamati ya Matayarisho ya Mkutano wa Mapitio ya Mapatano ya Durban, waliokutana Geneva, Ijumatatu wamekubaliana kuitisha kikao hicho Geneva mwezi Aprili, 2009 ambapo wajumbe wa kimataifa wanatarajiwa kuzingatia hatua za kuchukuliwa, kukabiliana, kwa nguvu moja, na masuala sugu ya ubaguzi na chuki za wageni. Matatizo haya bado yanaendelea kusumbua umma wa kimataifa katika karne tuliomo hivi sasa.