Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WHO kupiga vita unywaji pombe haribifu na vileo

WHO kupiga vita unywaji pombe haribifu na vileo

Kikao cha 61 cha Baraza Kuu la Shirika la Afya Duniani (WHO) ambacho karibuni kilikamilisha mijadala ya wiki moja mjini Geneva, Uswiss kilifanikiwa kupitisha azimio muhimu, liliopendekeza Mataifa Wanachama kutayarisha mradi wa mwongozo utakaotumiwa katika zile juhudi za kuzuia, na kudhibiti bora matumizi haribifu ya unywaji wa vileo na pombe.