Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utunzaji wa viumbe anuwai unahimizwa na UM kwa natija za wote kimataifa

Utunzaji wa viumbe anuwai unahimizwa na UM kwa natija za wote kimataifa

KM Ban Ki-moon na Raisi wa Baraza Kuu Srgjan Kerim wametoa onyo la pamoja wiki hii lenye kutahadharisha kwamba bila ya walimwengu kutunza mazingira ya viumbe na uhai anuwai, matokeo yake yatasababisha athari mbaya kimaisha, hali ambayo itaharibu na kuchafua pakubwa shughuli za uchumi, huduma za maendeleo na zile juhudi za kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa, takriban kote ulimwenguni. Onyo hili liliwasilishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira, Achim Steiner, kwa niaba ya KM na Raisi wa Baraza Kuu kwenye mkutano wa kusailia sera za kutunza kipamoja viumbe anuwai, unaofanyika mjini Bonn, Ujerumani.