Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utaalamu na mahema kufadhiliwa Afrika Kusini na UNHCR kwa waathiriwa wa hujuma za chuki

Utaalamu na mahema kufadhiliwa Afrika Kusini na UNHCR kwa waathiriwa wa hujuma za chuki

Msemaji wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) Geneva, Ron Redmond alipokutana na waandishi habari wa kimataifa Ijumaa aliripoti ya kuwa taasisi yao imepeleka misaada ya dharura Afrika Kusini itakayochangia juhudi za Serikali katika kuwahudumia kihali maelfu ya waathiriwa wageni waliong\'olewa makwao baada ya kushambuliwa kibaguzi karibuni nchini humo.~