BU limeongeza muda wa vikwazo dhidi ya majeshi ya mgambo katika JKK
Ijumatatu, asubuhi, kwa saa za New York, Baraza la Usalama limepitisha, kwa kauli moja, azimio nambari 1807 (2008) ambapo wajumbe wa Baraza walipendekeza muda wa mamlaka ya ile Tume ya Wataalamu wanaofuatilia utekelezaji wa vikwazo vya silaha dhidi ya makundi ya wanamgambo katika JKK uendelezwe hadi Disemba 31 (2008).