Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM waadhimisha Siku ya Kuhadharisha juu ya Ugonjwa wa Akili wa Watoto (Autism)

UM waadhimisha Siku ya Kuhadharisha juu ya Ugonjwa wa Akili wa Watoto (Autism)

Ijumatano, tarehe 02 Machi 2008 iliadhimishwa na UM, kwa mara ya kwanza kihistoria, ni Siku ya Kuongeza Hisia za Kimataifa kuhusu Ugonjwa wa Akili wa Watoto (Autism). Risala ya KM ya kuihishimu siku hii ilipongeza ujasiri wa watoto waliodhuiwa na maradhi haya ya akili, na pia wazee wao ambao kila siku "hukabiliana na ulemavu wa vizazi vyao kwa mchanganyiko wa nia thabiti, kipaji cha kubuni na matarajio ya kutia moyo." Baraza Kuu la UM lilipitisha mwaka jana mnamo mwezi Disemba 2007 azimio la kuifanya tarehe 2, kila mwaka, kuwa ni Siku ya Kuongeza Hisia za Kimataifa kuhusu Ugonjwa wa Akili wa Watoto (Autism). Maradhi haya humnyima mtoto anayepatwa nayo uwezo wa kuwasiliana na wenziwake, na hushindwa kuendeleza uhusiano wa kijamii, na mara nyingi watoto huonesha tabia isiyo ya kikawaida na inayofurutu ada.