Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

FAO kutabiri ongezeko la mavuno ya mpunga mwaka huu

FAO kutabiri ongezeko la mavuno ya mpunga mwaka huu

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limetabiri kwenye ripoti iliotolewa Ijumanne, kwamba mavuno ya mpunga mwaka huu yataongezeka kwa jumla ya asilimia 1.8, kiwango ambacho ni sawa na tani milioni 12 ziada za mpunga. Muongezeko huu utashuhudiwa zaidi katika nchi za Asia zinazopandisha nafaka hizo – mathalan, Bangladesh, Uchina, Bara Hindi, Indonesia, Myanmar na pia Phillippines na Thailand. Kadhalika uzalishaji wa mpunga unatarajiwa kuongezeka katika Afrika, Amerika ya Kusini na mataifa wanachama wa Umoja wa Ulaya, lakini katika Ujapani mavuno ya mpunga yatateremka, ikiwa moja ya mataifa machache ambayo bei za uzalishaji wa mpunga ziliporomoka mwaka jana.