Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WMO yasisitiza 'Afrika itahitajia vifaa vya kisasa kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa'

WMO yasisitiza 'Afrika itahitajia vifaa vya kisasa kudhibiti mabadiliko ya hali ya hewa'

Michel Jarraud, KM wa Shirika la UM juu ya Upimaji wa Hali ya Hewa Duniani (WMO) aliwaambia wajumbe waliohudhuria kikao kinachozingatia masuala ya fedha na uchumi katika Afrika, kinachofanyika sasa hivi Addis Ababa, Ethiopia, kwamba bara la Afrika linahitajia kufadhiliwa kidharura uwezo na vifaa vya kisasa ili kudhibiti bora mabadiliko ya hali ya hewa.