Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM Ban apongeza kufanywa sheria ya kimataifa Mkataba wa Haki za Walemavu

KM Ban apongeza kufanywa sheria ya kimataifa Mkataba wa Haki za Walemavu

KM Ban Ki-moon amepongeza tukio la kihistoria liliojiri Alkhamisi ambapo Mkataba juu ya Haki za Walemavu ulifanywa rasmi kuwa chombo cha sheria ya kimataifa baada ya Ecuador kuwa taifa la 20 kutia sahihi amana ya kuridhia Mkataba huo. Tangu tarehe 30 Machi 2007 nchi 126 zilitia sahihi Mkataba, na nchi 71 pia zimeidhinisha Itifaki ya Hiyari ya Mkataba itayoruhusu watu binafsi pamoja na makundi kuwa na haki ya kusaidiwa kihali.