Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IAEA kutathminia usalama wa viwanda vya nyuklia kwenye vikao vitatu tofauti

IAEA kutathminia usalama wa viwanda vya nyuklia kwenye vikao vitatu tofauti

Shirika la UM juu ya Huduma za Amani za Nishati ya Nyuklia (IAEA) linatarajiwa Ijumatano, tarehe 09 Aprili, kuanzisha vikao vitatu tofauti kutathminia usalama wa viwanda vinavyozalisha nishati za nyuklia ulimwenguni. Vikao hivi vitajumuisha wataalamu wa kutoka vyuo vikuu, viongozi wa viwanda vya kimataifa na vile vile magwiji wanaohusika na mashirika yanayosimamia matumizi salama ya viwanda vya nyuklia.