KM ameanza ziara rasmi katika Shirikisho la Urusi
KM Ban Ki-moon leo ameanza rasmi ziara ya siku tatu kwenye Shirikisho la Urusi ambapo anatarajiwa kusailia na viongozi wa taifa hilo, wakijumuisha Raisi Vladimir Putin pamoja na Raisi Mteule Dmitry Medvedev, masuala yanayohusu hali katika Kosovo, na mpango wa amani juu ya Mashariki ya Kati, hasa ilivyokuwa Urusi imependekeza kuandaa mkutano maalumu wa kuzingatia suala hilo.