Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF kuipongeza Afrika Kusini kwa sheria mpya inayolinda haki za watoto

UNICEF kuipongeza Afrika Kusini kwa sheria mpya inayolinda haki za watoto

Shirika la Mfuko wa Maendeleo ya Watoto (UNICEF) limepongeza utiaji sahihi wa sheria mpya Afrika Kusini iliokusudiwa kulinda na kutunza haki za watoto, kitendo ambacho kilitafsiriwa kupiga \'hatua kuu\' kimaendeleo na kuhakikisha ustawi na hali njema kwa raia vijana nchini humo.

Marekibisho ya Sheria kwa Watoto yaliofanyika Afrika Kusini ni "sheria mpya ya jumla inayolingana sawa na vifungu vya Mkataba wa UM juu ya Haki ya Mtoto" kwa mujibu wa mwakilishi mkaazi wa UNICEF Afrika Kusini, Macharia Kamau.