Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM apendekeza mifumko ya bei za chakula idhibitiwe haraka

KM apendekeza mifumko ya bei za chakula idhibitiwe haraka

Kwenye hotuba aliowasilisha hapo jana kwenye kikao kilichoandaliwa na Baraza la ECOSOC pamoja na taasisi za Bretton Woods ~ yaani Benki Kuu ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani ~ na kujumuisha pia Shirika la Biashara na Maendeleo (UNCTAD) na Shirika la Biashara Ulimwenguni (WTO), KM Ban alitoa mwito maalumu ulioyakumbusha Mataifa Wanachama kwamba kunahitajika kuchukuliwe hatua za haraka, za muda mfupi na muda mrefu, kuhakikisha tatizo la mgogoro wa bei za chakula duniani linadhibitiwa kidharura.