Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF itashindwa kuhudumia watoto chakula baada ya bei za nafaka kuongezeka

UNICEF itashindwa kuhudumia watoto chakula baada ya bei za nafaka kuongezeka

Kadhalika, Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) limetangaza kwamba kwa sababu ya kupanda kwa bei za chakula duniani, shirika litashindwa kuhudumia chakula watoto katika seghemu mbalimbali za dunia, hasa wale wanaoishi katika mataifa yanayoendelea, watoto ambao kawaida hutegemea kukirimiwa misaada ya chakula kutoka mashirika ya kimataifa kwa madhumuni ya kujikinga na tatizo kuu la utapia mlo.