Upungufu wa chakula Korea Kaskazini unahatarisha maisha ya umma, kutahadharisha WFP
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetoa onyo maalumu leo kwamba Jamhuri ya Kidemokrasia ya Umma wa Korea (DPRK) inakabiliwa na tatizo hatari la upungufu wa chakula kwa sababu ya mavuno haba, hali ambayo ilitokana na matatizo kadha, ikiwemo maafa ya mafuriko yaliotukia nchini humo mwaka jana.~