Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

EthiopiaEritrea: KM anaonya ulinzi wa UM mipakani ukikomeshwa utaruhusu uhasama kurejea

EthiopiaEritrea: KM anaonya ulinzi wa UM mipakani ukikomeshwa utaruhusu uhasama kurejea

KM wa UM Ban Ki-moon amewasilisha ripoti maalumu majuzi kuhusu operesheni za Shirika la UM juu ya Ulinzi wa Amani Mipakani Ethiopia/Eritrea (UNMEE), Ripoti imependekeza kwa jumuiya ya kimataifa kuzingatia kidharura changuzi nne muhimu, kusailia kama huduma za amani bado zinahitajika kuendelezwa kwenye eneo la uhasama katika Pembe ya Afrika au zisitishwe, hususan baada ya wenye madaraka Eritrea kuamua kuweka vikwazo kwenye upande wao wa mpaka, hali ambayo ilikwamisha na kozorotisha operesheni za amani za UM.

Sikiliza maelezo kamili kwenye idhaa ya mtandao.