Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tume ya Kudumu ya Wenyeji wa Asili yakutana Makao Makuu katika kikao cha mwaka

Tume ya Kudumu ya Wenyeji wa Asili yakutana Makao Makuu katika kikao cha mwaka

Kikao cha Saba cha Tume ya Kudumu ya UM juu ya Masuala ya Haki za Wenyeji wa Asili, kitakachochoendelea kwa wiki mbili, kilifunguliwa rasmi Ijumatatu, Aprili 21 kwenye Makao Makuu mjini New York. Mada ambayo inatarajiwa kupewa umuhimu zaidi mwaka huu ni ile inayoambatana na athari za mabadiliko ya hali ya hewa kwenye tamaduni maumbile na namna inavyodhuru uwezo wa wananchi wa asili kujipatia riziki za kuendesha maisha.