Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtaalamu Huru juu ya Haki za Binadamu katika Usomali alaani vikali mauaji ya kihorera ya raia nchini

Mtaalamu Huru juu ya Haki za Binadamu katika Usomali alaani vikali mauaji ya kihorera ya raia nchini

Ghanim Alnajjar, Mkariri Mtaalamu Huru juu ya Haki za Binadamu katika Usomali, amenakiliwa akisema mjini Geneva kuwa amechukizwa na kushtushwa sana kwa kuongezeka vurugu na kuharibika kwa haki za kimsingi za raia nchini Usomali, kufuatilia mapigano makali yaliozuka majuzi kati ya vikosi vya Serikali ya Mpito, inayosaidiwa na Jeshi la Ethiopia, dhidi ya vikundi wapinzani wa serikali.