Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ILO inasema udhibiti bora makazini huokoa maisha

ILO inasema udhibiti bora makazini huokoa maisha

Shirika la UM juu ya Haki za Wafanyakazi (ILO) limetoa ripoti mpya yenye kuonyesha watu milioni 2.2 hufariki kila mwaka katika dunia kwa sababu ya ajali zinazoambatana na ajira pamoja na maradhi wanayopata makazini. ILO imependekeza taratibu za usimamizi kwenye mahali pa kazi zirekibishwe ili kuwawezesha viongozi na mameneja kutambua na kubashiria mapema zaidi hatari ziliopo na kuzidhibiti mapema kabla hazijasababisha vifo vya ajali.