Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF inaonya, bei kubwa ya chakula inahatarisha maisha ya watoto

UNICEF inaonya, bei kubwa ya chakula inahatarisha maisha ya watoto

Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) limeripoti kuwa na wasiwasi kuhusu uhaba wa lishe kwa wanawake na watoto wa mataifa yanayoendelea, kwa sababu ya muongezeko mkubwa wa bei za chakula duniani katika kipindi cha karibuni. UNICEF inakhofia tatizo la kupanda kwa kasi kwa bei ya chakula duniani, kunachochea na kukithirisha athari mbaya za kiuchumi na kijamii katika mataifa masikini, ambapo kabla ya mgogoro huo kuzuka familia hizo zilikuwa zikitumia asilimia 70 ya pato lao kununua chakula, na inakhofiwa hizi ndio jamii zitakazoumizwa na kudhurika zaidi na kupanda kwa bei ya chakula katika soko la kimataifa.