Utumiaji mabavu na vurugu la Zimbabwe kumshtusha Kamishna wa Haki za Binadamu
Ijumapili, Louise Arbour, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu alitoa taarifa maalumu mjini Geneva iliyoelezea kushtushwa sana na ripoti aliyopokea kuhusu kuendelea kwa vitendo vya mabavu na hali ya vurugu katika Zimbabwe kufuatia uchaguzi wa karibuni.