Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM ameshtumu mauaji katika Tarafa ya Ghaza

KM ameshtumu mauaji katika Tarafa ya Ghaza

KM Ban Ki-moon ameshtumu upotezaji wa maisha ya raia uliotukia mapema Ijumatatu kwenye Tarafa ya Ghaza, msiba ambao pia ulisababisha vifo kadha, ikijumuisha vifo vya mama mmoja na watoto wake wanne. Kwa mujibu wa taarifa iliotolewa na Ofisi ya KM kuhusu tukio hili, vikosi vya Israel vilivyokuwa vikiendeleza operesheni zake katika Ghaza vilikumbushwa tena dhamana walionayo, chini ya sheria za kiutu za kimataifa, ya kuhifadhi na kuwahami raia walionaswa kwenye mazingira ya mapigano.