Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakariri wa haki za binadamu wana wasiwasi na hali Zimbabwe

Wakariri wa haki za binadamu wana wasiwasi na hali Zimbabwe

Wakariri sita wa UM wanaohusika na haki za binadamu wamenakiliwa wakisema wana wasiwasi kuhusu kuporomoka kwa haki za binadamu na kuzuka kwa hali ya mtafaruku Zimbabwe kufuatia uchaguzi wa raisi na bunge uliofanyika March 29. Wataalamu hawa wanahusika na masuala ya mauaji ya kihorera, udhalilishaji wa wanawake, haki ya kupata makazi, haki ya uhuru wa kusema na hifadhi kinga dhidi ya mateso. Kwenye ripoti iliotolewa Geneva wataalamu hawo walibainisha kwamba wamepokea ripoti zenye kuaminika, zilizoelezea ya kuwa tangu uchaguzi ulipomalizika nchini Zimbabwe, vitendo vya vitisho na uonevu vilikithiri dhidi ya wale raia waliodhaniwa na kutuhumiwa kupigia kura, au kuunga mkono, chama cha upinzani cha Movement for Democratic Change (MDC) na wale waliohusika na Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe (ZEC).