Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ICC kutangaza hati rasmi ya kumshika kiongozi wa CNDP katika JKK

ICC kutangaza hati rasmi ya kumshika kiongozi wa CNDP katika JKK

Mahakama ya Kimataifa juu ya Jinai ya Halaiki (ICC) imetoa hati rasmi ya kumkamata Bosco Ntaganda, kiongozi wa jeshi la mgambo la CNDP, baada ya kutuhumiwa, katika siku za nyuma, kuwalazimisha watoto wenye umri mdogo kujiunga na kundi lao na kushiriki kwenye mapigano, hasa katika wilaya ya utajiri mkubwa wa maadini ya Ituri, iliopo mashariki ya JKK; na alituhumiwa kurudia vitendo hivyo pia katika jimbo la Kivu Kaskazini.