Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali ya Zimbabwe inasailiwa na BU

Hali ya Zimbabwe inasailiwa na BU

Naibu KM juu ya Masuala ya Kisiasa, Lynn Pascoe Ijumanne alizungumzia hali Zimbabwe na wajumbe wa Baraza la Usalama. Baadaye alikutana na waandishi habari wa kimataifa ambao aliwabainishia taarifa isemayo kwamba UM upo tayari kusaidia kwa kila njia, kwa kupitia diplomasiya ya kikanda, ili kuharakisha suluhu ya kuridhisha kwa mzozo uliojiri Zimbabwe kufuatilia uchaguzi wa taifa.