Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UNHCR azuru kambi za wahamiaji Afrika Mashariki

Mkuu wa UNHCR azuru kambi za wahamiaji Afrika Mashariki

Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR), Ijumatatu alianza ziara ya siku nane kutembelea Tanzania na Uganda, ambapo anatazamiwa kufanya mapitio kuhusu namna shughuli zinavyoendelezwa kwenye mataifa haya mawili katika kuwasaidia kihali wahamiaji muhitaji waliopo huko.